Home » » maajabu....../////// picha za kwanza za mtu aliyeliwa sura yake akiwa hai.....

maajabu....../////// picha za kwanza za mtu aliyeliwa sura yake akiwa hai.....

tangazo
Madactari nchini Marekani wametoa picha za mwanzo za mwanaume ambaye sura yake pamoja na pua yake ililiwa na mtu aliyekuwa amepagawa na madawa mapya ya kulevya yanayomfanya mtu awe na hasira kali na mwenye kutaka kujiua.

 Baada ya mei 26 mwaka huu, Ronald Poppo mwenye umri wa miaka 65, Mzee aliyekuwa hana makazi maalumu akilala mitaani, kushambuliwa na kuliwa sura yake alipokuwa amelala pembeni ya stesheni, madaktari wa hospitali ya Miami nchini Marekani wametoa picha na video za Poppo wakisema kuwa anaendelea vizuri na matibabu.

Katika tukio hilo, Rudy Eugene, aliyekuwa na umri wa miaka 31, akiwa uchi wa mnyama huku ikisemekana akiwa amepagawa na madawa mapya ya kulevya yanayoitwa "Bath Salts" au "Ivory Wave", "Purple Wave" au "Vanilla Sky", alimshambulia Poppo ambaye naye alikuwa uchi wakati wa tukio.

Eugene aliutafuna uso wa Poppo na aliendelea kuutafuna pamoja na kupigwa risasi na polisi ili kumfanya asiendelee na shambulio hilo. Polisi walilazimika kumpiga risasi 12 Eugene ndipo alipofariki na shambulio hilo ndipo lilipofikia kikomo.

Lakini hadi shambulio hilo linaisha, asilimia 80 ya sura ya Poppo ilikuwa imeishaliwa. Alikuwa ameishaliwa pua yake yote, jicho lake moja huku jicho jingine likiwa limeharibiwa vibaya sana. Madaktari wanahofia Poppo huenda akapoteza jicho hilo lililobaki akawa kipofu.

Sura yake iliharibiwa vibaya sana kiasi cha kuwafanya madaktari wamfanyie operesheni kadhaa za kurekebisha sura yake.

Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa Eugene ambaye hakuwa na historia ya uhalifu, alikuwa amelewa madawa hayo mapya ya kulevya ambayo humfanya mtu awe mwenye hasira kali, mwenye kutamani kujiua na mwenye kufikiria vitu vya ajabu ajabu.

Madawa hayo ya kulevya ambayo hutengenezwa mitaani kutokana na mchanganyiko wa kemikali yanasemekana pia kumfanya mtu awe anatamani kula nyama za watu. Hivi karibuni babu mmoja wa nchini Marekani aliyetumia madawa hayo ya kulevya alitiwa mbaroni baada ya kutishia kuwatafuna maafisa wa polisi.

Wiki tatu baada ya tukio hilo, madaktari wametoa picha na video ya Poppo wakisema anaendelea vizuri na matibabu.

Tupe Maoni yako!

KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DODOSO - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger