Home » , » IDD AMINI APIGWA CHINI MEDALI ZA HESHIMA KWA MARAIS WALIOWAHI KUIONGOZA UGANDA

IDD AMINI APIGWA CHINI MEDALI ZA HESHIMA KWA MARAIS WALIOWAHI KUIONGOZA UGANDA

tangazo

Idd Amin Dada.

Mwenyekiti wa kamati ya Taifa ya Tuzo na Medali nchini Uganda Jenerali Elly Tumwine ameweka wazi kuwa katika tuzo za heshima zilizotolewa kwa marais waliowahi kuingoza nchi hiyo pamoja na watu wengine ambao mchango wao unatambulika..

 Aliyewahi kuwa rais nchini humo Hayati Field Marshal Idi Amin Dada hakupata heshima kwa sababu aliacha urithi wa mfumo mbaya wakati wa uongozi wake.

Marais wote wametunukiwa Medali za Miaka 50 ya Uhuru wa Uganda wakati wa maadhimisho ya sherehe za chama cha NRM kutimiza miaka 27 yaliyofanyika wilaya Kasese, ambapo rais Yoweri Museveni alipokea medali ya, sambamba na watu wengine 43.
Jumla ya watu 3,500 nchini Uganda watapokea tuzo hiyo ambayo inawatambua mtu mmoja mmoja kwa mchango wake katika kutoa huduma na uzalendo kwa nchi hiyo tangu ilipopata uhuru.

Jenerali Tumwine amesema Amini hakutambuliwa kwa sababu ya mfumo mbaya alioutumia wakati wa uomgozi wake.

Amini alikuwa rais wa Uganda kutoka mwaka 1971 hadi 1979 ambapo aliingia madarakani kwa kupindua serikali ya Milton Obote Januari 1971.

Marais wengine wote waliopita wakiwemo Sir Edward Mutesa, Obote, Yusuf Lule, Godfrey Lukongwa Binaisa na Gen. Tito Okello, wametunukiwa medali hizo za heshima.

Tupe Maoni yako!

KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DODOSO - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger