Home » » WAFANYAKAZI WA SERIKALI GAMBIA SASA KUFANYA KAZI KWA SIKU 4 TU KWA WIKI KWA MSHAHARA ULE ULE

WAFANYAKAZI WA SERIKALI GAMBIA SASA KUFANYA KAZI KWA SIKU 4 TU KWA WIKI KWA MSHAHARA ULE ULE

tangazo


Serikali ya Gambia imetambulisha mfumo mpya wa siku za kufanya kazi kwa wafanyakazi wa serikali ambapo sasa watafanyakazi kwa siku nne tu, huku siku ya Ijumaa nayo ikiwa siku ya mapumziko.

Rais wa nchi hiyo Yahya Jammeh (pichani) amesema wananchi wa Gambia ambao wengi wao ni waislamu sasa watapata muda zaidi kusali, kushiriki shughuli za kijamii na kulima mashamba yao.

Kwa mujibu wa taarifa ni kuwa sasa wananchi wa Gambia wanapaswa kuingia mashambani kupanda mazao ya chakula na kutumia chakula hicho ili taifa hilo liwe tajiri.

Rais huyo amesema mishahara haitapunguzwa kwa sababu kwa siku hizo nne watu watafanyakazi zaidi ya saa za kawaida ili kufidia siku ya tano.

Shule za serikali sasa hazitafunguliwa tena Ijumaa, ila sekta binafsi zitafanyakazi zao ila hazitaweza kufanya biashara yeyote na serikali siku hiyo.

Rais Jammeh mwenye historia ya kuwa na tabia za kustaajabisha hajawapa wananchi wa Gambia muda wa kujiandaa kwa mfumo huo mpya.

Rais Jammeh aliingia madarakani kwa mapinduzi yaliyomwaga damu mwaka 1994.


Tupe Maoni yako!

KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DODOSO - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger